Saturday 7 September 2013

WANAFUNZI WABADILISHA CHUMA CHAKAVU KWA MADAFTARI

Ule usemi kwamba ukitaka elimu huna budi kuitafuta "popote na kwa gharama yoyote" umewaingia wanafunzi wa shule ya Msingi Mwampunga Bule iliyopo kata ya Mishepo wilaya ya Shinyanga vijijini waliolazimika kubadilishana vyuma chakavu na wafanyabiashara wa bidhaa hizo ili kupata mahitaji yao ya shule.

Hatua hiyo imekuja baada ya baadhi ya wazazi kukosa mwamko wa elimu hivyo kuacha kuwahudumia watoto wao mahitaji yao ya shule ambapo biashara hiyo inawasaidia wanafunzi hao kupata mahitaji muhimu kama vile madaftari, kalamu pamoja na mabegi ya kubebea madaftari.

Njia hii imebuniwa na baadhi ya wanafunzi wanaopenda elimu, jambo ambalo pia limeungwa mkono na walimu wa shule hiyo baada ya kuona ni mkombozi kwa wanafunzi hao.

No comments:

Post a Comment